Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF)

UCSAF YAKAGUA MAABARA YA KOMPYUTA SHULE YA SEKONDARI YA WASICHANA MSALATO

Imewekwa: 23 January, 2025
UCSAF YAKAGUA MAABARA YA KOMPYUTA SHULE YA SEKONDARI YA WASICHANA MSALATO

Bodi ya Wakurugenzi ya Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF), ikiongozwa na Mwenyekiti wake, Mhe. Balozi Valentino Longino Mlowola, imefanya ziara muhimu katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Msalato, iliyopo jijini Dodoma, kwa lengo la kukagua na kupata taarifa ya matumizi ya maabara ya kompyuta (Computer Lab) iliyojengwa na UCSAF ikiwa ni utekelezaji wa mradi wa kuunganisha shule za umma na mtandao wa intaneti.

Kupitia mradi huo UCSAF huzipatia shule za umma vifaa vya TEHAMA kwa  lengo la kusaidia wanafunzi katika kujifunza na kuwajengea uwezo wa kutumia vifaa hivyo ili kukabiliana na changamoto za ulimwengu wa sasa wa kidijitali.

Je, una swali lolote kuhusu Mfuko wa Mawasiliano kwa Wote (UCSAF)? Faili Maoni na Malalamiko! Universal Communications Service Access Fund Ripoti Hapa
Tuma malalamiko na mrejesho wako