Ujenzi wa Vituo vya TEHAMA Zanzibar.

  • 14 September, 2021
Ujenzi wa Vituo vya TEHAMA Zanzibar.

UCSAF imejenga vituo 10 vya TEHAMA Zanzibar ambapo Vituo VINNE (4) vimejengwa Pemba na Vituo SITA (6) vimejengwa Unguja. Kwa mwaka wa fedha 2021/22, UCSAF ilipanga kujenga kituo kingine kimoja cha TEHAMA ambapo kituo hicho kimejengwa katika eneo la Fumba, Mkoa wa Mjini Magharibi Wilaya ya Mjini, ambapo ujenzi wa kituo ulikamilika katika kipindi cha Julai – Disemba, 2022 na kuzinduliwa tarehe 26 Oktoba, 2022 na Mhe. Dkt. Hussein Ali Hassan Mwinyi, Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar.

Kukamilika kwa kituo hiki kumefanya Wilaya zote 11 kwa upande wa Pemba na Unguja kuwa na kituo cha TEHAMA. Vituo hivi vinasaidia kutoa mafunzo ya TEHAMA, vinatumika kutoa huduma za intaneti kwa wananchi mbalimbali na huduma zingine mbalimbali za TEHAMA.